Friday, April 20, 2012

IYA MUST GO-ROGER MILLA

MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa Cameroon, Roger Milla amesema kuwa rais wa Shirikisho la Soka la nchi hiyo Iya Mohammed anatakiwa kujiuzulu wadhfa huo. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Yaounde, Milla ambaye amewahi kuchukua tuzo ya mchezaji bora wa Afrika mwaka 1987 amesema kuwa Mohammed pamoja na viongozi wote wa shirikisho hilo ndio chanzo cha kiwango kibovu kilichoonyeshwa na timu ya taifa ya nchi hiyo katika siku za karibuni.
Cameroon ambao wameshawahi kunyakuwa taji la michuano ya Afrika mara nne walishindwa kufuzu michuano hiyo iliyochezwa mapema mwaka huu ambayo iliandaliwa na nchi majirani zao Gabon na Equatorial Guinea. Kutokana na matatizo hayo Milla na baadhi ya wachezaji wa zamani wan chi hiyo wamekaa kikao cha siri ilin kuangalia uwezekano wa kuuondoa uongozi wa Mohammed madarakani wakiamini ndio njia pekee ya kuihakikishia kikosi cha nchi hiyo kufuzu michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani pamoja na michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2014. Kundi hilo pia linadai kutenguliwa mara moja kwa adhabu aliyopewa nahodha wa kikosi cha timu ya nchi hiyo Samuel Eto’o na kusema kuwa wanahitaji wachezaji wake bora wote kwa ajili ya changamoto iliyopo mbele yao. Shirikisho la soka la nchi hiyo lilimfungia Eto’o miezi nane kutokana na kuongoza mgomo ambao ulipelekea kikosi cha nchi hiyo kukosa mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Algeria Octoba mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment