Tuesday, April 24, 2012

DENMARK BANS PLAYERS FROM TWEETING.

SHIRIKISHO la Soka nchini Denmark limesema kuwa wachezaji wa timu ya taifa ya nchi hiyo hawataruhusiwa kutumia mitandao ya kijamii wakati wa michuano ya Ulaya itakayofanyika June mwaka huu. Golikipa wa kikosi cha nchi hiyo Thomas Sorensen amesema kuwa ni aibu kwa wachezaji kutowasiliana na mashabiki wao kuwajuza wanachofanya bila kuweka wazi mikakati yao. Msemaji wa shirikisho hilo Lars Behrendt amesema kuwa kocha wa timu hiyo amefanya hivyo ili wachezaji wa timu hiyo waweze kuweka mawazo yao katika mchezo huo na sio kitu kingine. Behrendt aliendelea kusema wachezaji wataruhusiwa kuwasiliana na mashabiki kupitia mtandao wa kijamii wa timu hiyo ambao utafunguliwa na sio wa mchezaji binafsi ingawa suala hilo limepingwa na Waziri wa michezo wa nchi hiyo Uffe Elbaek akisema kuwa unawanyima wachezaji hao uhuru wa kuongea.

No comments:

Post a Comment