Friday, April 27, 2012

GUARDIOLA KUIKACHA BARCELONA MWISHONI MWA MSIMU HUU.

MENEJA wa timu ya Barcelona, Pep Guardiola anatarajiwa kuacha kuinoa klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu baada ya kukataa kuongeza mkataba wake. Mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Hispania alikutana na Rais wa klabu hiyo Sandro Rosell na Mkurugenzi wa Michezo Andoni Zubizarreta jana na kuwaeleza uamuzi wake huo aliouchukua wakupumzika za mambo ya soka kwa muda. Viongozi hao wa Barcelona walimuomba Guardiola kuangalia upya uamuzi wake kwani bado walikuwa wakimuhitaji kuendelea kuinoa klabu hiyo lakini kocha huyo ambaye ana umri wa miaka 41 ameshaamua kuiacha klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu. Guardiola ambaye alikiongoza kikosi cha Barcelona kushinda mataji 13 toka alipochukua mikoba mwaka 2008 tayari ameshawapa taarifa wachezaji kuhusu kuondoka kwake katika mkutano uliofanyika asubuhi leo ambao baadae anatarajiwa kuongea na vyombo vya habari.

No comments:

Post a Comment