Friday, April 27, 2012

WAKAGUZI FIFA KUITEMBELEA MIJI MIWILI BRAZIL.

WAKAGUZI wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA wameanza ziara nchini Brazil kukagua miji miwili ambayo inaweza kuwa wenyeji wa michuano ya Kombe la Confederations inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi mwaka kesho. Wakaguzi hao wanatarajiwa kutembelea miji ya Salvador na baadae Recife ili kuangalia maendeleo ya ujenzi miundo mbinu pamoja na viwanja vitakavyotumika kwa ajili ya michuano hiyo. Baada ya ziara hiyo wakaguzi hao wanatarajia kuandaa taarifa ambayo wataiwasilisha kwa viongozi wa FIFA pamoja na Kamati ya Maandalizi ya Kombe la Dunia ya nchi hiyo na maamuzi yatatolewa kama miji hiyo itapewa nafasi ya kuandaa michuano hiyo inayotarajiwa kufanyika Juni mwakani. Miji ya Salvador na Recife kama ikipitisha itaungana na miji mingine minne ambayo ni Rio de Janeiro, Brasilia, Belo Horizonte na Fortaleza ambayo yenyewe tayari imeshapitishwa kuandaa michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment