Friday, April 27, 2012

HISPANIA YATUPIA TIMU MBILI FAINALI EUROPA LEAGUE.

TIMU za Athletic Bilbao na Atletico Madrid zote za Hispania zimefanikiwa kutinga katika hatua ya fainali ya michuano ya Kombe la Ligi la Ulaya maarufu kama Europa League baada ya kushinda michezo yao ya pili ya nusu fainali iliyochezwa jana usiku. Bilbao ilifanikiwa kutinga katika hatua hiyo baada ya kifunga mabao 3-1 timu ya Sporting Lisbon ya Ureno hivyo kufanikiwa kusonga mbele kwa jumla ya mabao 4-3 katika michezo yote miwili waliyocheza. Kwa upande wa Atletico wao walitinga katika hatua hiyo baada ya kufanikiwa kuifunga Valencia bao 1-0 na hiyo kusonga mbele kwa jumla ya mabao 5-2 katika michezo yao miwili waliocheza. Bilbao ambao pia walizitoa timu za Manchester United na Schalke, itakuwa inacheza fainali yake ya kwanza kwenye michuano hiyo ya Ulaya toka mwaka 1977 wakati walipofungwa na Juventus. Timu hizo zinatarajiwa kukutana katika mchezo wa fainali utakaochezwa Mei 9 mwaka huu katika Uwanja wa Bucharest, Romania.

No comments:

Post a Comment