Friday, April 27, 2012

UINGEREZA KUJIFUA NA BRAZIL OLIMPIKI.

TIMU ya soka ya Olimpiki ya Uingereza inatarajiwa kucheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Brazil kwa ajili kujipima nguvu kabla ya kuanza kwa michuano hiyo ambayo wanashiriki kwa mara ya kwanza baada ya miaka 52. Kikosi hicho ambacho kiko chini ya kocha Stuart Pearce, kitaingia uwanjani kupambana Brazil Julai 20 katika Uwanja wa Riverside iliopo jijini Middlesbrough kabla ya kuanza kampeni ya kutafuta medali ya dhahabu wakati watapocheza na Senegal Julai 26 katika Uwanja wa Old Trafford jijini Manchester. Brazil ambao ni mabingwa mara tano wa Kombe la Dunia lakini hawajawahi kushinda medali ya dhahabu katika michuano ya Olimpiki wenyewe wataanza kampeni yao kwa kucheza na Misri tarehe kama hiyo katika Uwanja wa Millennium uliopo jijini Cardiff, Wales. Katika michuano ya soka kwenye Olimpiki timu za wanaume zinaruhusiwa kuwa na vijana chini ya miaka 23 huku kila timu ikiruhusiwa wachezaji watatu ambao watakuwa wamezidi umri huo wakati kwa upande wa wanawake wenyewe wanaruhusiwa kuwa na wachezaji wao wa timu za taifa.

No comments:

Post a Comment