Wednesday, April 25, 2012

MARADONA ATISHIA KUIHAMA AL WASL.

KOCHA wa klabu ya Al Wasl, Diego Maradona ametishia kuihama klabu hiyo ya Umoja wa Falme za Kiarabu-UAE baada ya msimu huu wa Ligi Kuu ya nchi hiyo. Maradona amesema kuwa ana mpango wa kukutana na Ofisa Mkuu wa klabu hiyo wiki ijayo ili aweze kumuongeza kumuongeza fungu la kununua wachezaji ambao watamuwezesha kuiweka timu kiushindani zaidi kuliko hivi sasa. Mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Argentina ambaye alichukua mikoba ya kuinoa klabu hiyo Mei mwaka jana amesema kuwa kuondoka katika klabu hiyo hakumaanishi kwamba amepata timu nyingine bali anahisi klabu hiyo imevunja waliompa ya kununua wachezaji ambao atawahitaji. Hii sio mara ya kwanza kwa Maradona kutishia kusitisha mkataba na klabu hiyo kutokana na kutokuwa na wachezaji wazoefu kwani alitishia kuondoka Februari mwaka huu kutokana na pesa kidogo anayopewa kwa ajili kununua wachezaji.

No comments:

Post a Comment