Wednesday, April 25, 2012

PEARCE KUMFUATA BECKHAM MAREKANI.

KOCHA wa timu ya taifa ya Uingereza, Stuart Pearce anatarajiwa kusafiri kwenda Marekani kumuona mchezaji wa Los Angeles Galaxy David Beckham akicheza kabla ya kuamua kumuita mchezaji huyo katika michuano ya Olimpiki itakayofanyika jijini London. Beckham ni miongoni mwa wachezaji 80 ambao wako katika orodha ya kuteuliwa katika kikosi cha nchi hiyo ambacho kitashiriki michuano hiyo huku wachezaji ambao watahitajika katika orodha hiyo ni 18 tu. Mchezaji atakuwa na nafasi ya kumshawishi Pearce kumteua katika kikosi chake wakati kocha huyo atapotizama mchezo kati ya Galaxy na Seattle Sounders utakaofanyika Mei 2 mwaka huu. Beckham ambaye ni nahodha wa zamani wa Uingereza angependa kucheza michuano hiyo ya Olimpiki kabla ya kustaafu kucheza soka.

No comments:

Post a Comment