Wednesday, April 25, 2012

MOURINHO KUENDELEA KUINOA MADRID.

KOCHA wa Real Madrid, Jose Mourinho amesema kuwa angependa kubakia kuinoa klabu hiyo ambayo leo itakuwa ikitafuta nafasi kucheza fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich. Kwasasa kocha huyo mkataba wake unaishia mwaka 2014 na mara nyingi amekuwa akikataa kuthibisha kama ataendelea na klabu hiyo huku kukiwa na taarifa za kurejea katika klabu yake ya zamani ya Chelsea au Manchester City. Akihojiwa na waandishi wa habari kabla ya mchezo wao na Bayern Munich, Mourinho ambaye ni raia wa Ureno amesema kuwa anadhani ataendelea kuinoa klabu hiyo kwa kuwa hana sababu ya kuondoka. Ameendelea kusema kuwa atazungumza na wachezaji pamoja na viongozi wa klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu kama watamuhitaji kubakia katika klab u hiyo.

No comments:

Post a Comment