Wednesday, April 25, 2012

NILISTAHILI KADI NYEKUNDU-TERRY.

NAHODHA wa Chelsea, John Terry amesema kuwa alistahili kadi nyekundu wakati kikosi chake kilipotoa sare na mabao 2-2 na kufanikiwa kuingia fainali ya michuano ya Kombe la Klabu Bingwa ya Ulaya. Terry alionyeshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja dakika ya 37 na mwamuzi Cuneyt Cakir kutoka Uturuki ambaye alichezesha mchezo huo baada ua kumkwatua Alexis Sanchez kwa nyuma. Mchezaji huyo ambaye sasa atakosa mchezo wa fainali ya michuano hiyo itakayofanyika Mei 9 mwaka huu amesema kuwa anajutia kufanya kutendo hicho lakini akakiri kuwa hakudhamiria kama inavyoonekana katika picha za video. Chelsea pia itamkosa beki wake mwingine Branislav Ivanovic katika mchezo huo wa fainali utaofanyika jijini Munich, Ujerumani baada ya beki huyo kupewa kadi nyingine ya njano katika mchezo huo.

No comments:

Post a Comment