Thursday, April 26, 2012

MOURINHO WANTS CHELSEA FINAL VICTORY.

KOCHA wa klabu ya Real Madrid, Jose Mourinho anataka Chelsea iwafunge Bayern Munich katika mchezo wa fainali ya Kombe la Klabu Bingwa ya Ulaya baada ya timu yake kutolewa katika hatua ya nusu fainali kwa changamoto ya mikwaju ya penati. Chelsea ilifanikiwa kuingia katika hatua hiyo baada ya kufanikiwa kuifunga Barcelona, pamoja na kucheza wachezaji kumi karibu kipindi chote cha pili baada ya Terry kutolewa kwa kadi nyekundu. Mourinho amewahi kuinoa Chelsea kipindi cha nyuma amesema kuwa angependa timu hiyo washinde kombe hilo kwani walionyesha ushujaa mkubwa walipoweza kuwafunga Barcelona wakiwa pungufu. Pia aliongeza kuwa anajivunia kikosi chake pamoja na kutolewa katika michuano hiyo na sasa wanaelekeza nguvu zao katika kuhakikisha wananyakuwa Kombe la Ligi Kuu nchini Hispania. Bayern ambao watakuwa wakifukuzia taji lao la tano, watakuwa ni klabu ya kwanza katika historia ya michuano hiyo kucheza fainali ya michuano hiyo wakiwa uwanja wa nyumbani toka AS Roma walipofanya hivyo mwaka 1984 ingawa walifungwa na Liverpool kwa changamoto ya mikwaju ya penati.

No comments:

Post a Comment