Thursday, April 26, 2012

NILIMGWAYA CASILLAS KUPIGA PENATI YA PILI.

MSHAMBULIAJI wa Bayern Munich, Arjen Robben amekiri kuwa hakutaka kupiga penati katika mchezo wa pili wa nusu fainali ya michuano ya Klabu Bingwa ya Ulaya dhidi ya Real Madrid akidai kuwa golikipa Iker Casillas anamfahamu vyema. Robben alipiga penati ya kwanza dakika 27 na kufanikiwa kuirejesha timu yake katika mchezo baada ya kufungwa mabao mawili ya mapema na wapinzani na kupelekea mchezo huo kuamuliwa kwa changamoto ya mikwaju ya penati baada ya kufungana mabao 3-3 katika michezo miwili walioyokutana. Hatahivyo Robben alijitoa kupiga penati nyingine ilipofikia hatua hiyo akidai kuwa ingekuwa ni ngumu zaidi kwake kutokana na Casilas kumfahamu vizuri udhaifu wake kwa kuwa walicheza wote katika kipindi cha miaka miwili alipokuwa Madrid. Katika mchezo huo Bayern walifanikiwa kushinda mchezo huo kwa changamoto ya mikwaju ya penati ambapo sasa watacheza na Chelsea katika fainali itakayofanyika Mei 9 mwaka huu katika uwanja wao wa nyumbani wa Alianz Arena, jijini Munich.

No comments:

Post a Comment