Thursday, April 26, 2012

UEFA KUMJADILI TERRY.

KAMATI ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA inatarajia kukutana kumjadili nahodha wa klabu ya Chelsea, John Terry baada ya kutolewa nje katika mchezo wa nusu fainali ya michuano ya Klabu Bingwa ya Ulaya dhidi ya Barcelona, Jumanne. Kwa kadi hiyo aliyopewa Terry atakosa mchezo mmoja ambao utakuwa ni wa fainali itakayochezwa Mei 9 jijini Munich lakini kwa sheria za UEFA inaruhusu kamati ya nidhamu kuongeza adhabu ambayo anaweza kuitumikia katika michuano ijayo ya Ulaya msimu ujao. Chelsea itapata pigo kubwa baada ya Branislav Ivanovic, Raul Meireles na Ramires nao kukosa mchezo w fainali baada ya kufungiwa mchezo mmoja kwa kupewa kadi za njano kwenye michezo mitatu mfululizo kwenye michuano hiyo. Kamati hiyo inatarajiwa kukutana Mei 31 ili kujadili hatma Terry kuhusiana na sula lake hilo.

No comments:

Post a Comment