Thursday, April 26, 2012

WAAMUZI TISA KUTOKA AFRIKA KUCHEZESHA OLIMPIKI.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limetoa orodha ya waamuzi na wasaidizi watakaochezesha michuano ya Olimpiki jijini London ya soka kwa wanaume na wanawake. Waamuzi tisa kutoka Afrika ni miongoni jumla ya waamuzi 84 waliopo katika orodha hiyo kutoka nchi 36 ambao watachezesha michuano hiyo ambayo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi kati ya Julai 27 hadi Agosti 12 mwaka huu. Waamuzi sita kati ya hao wanatarajiwa kuchezesha soka kwa upande wa wanaume ambapo waamuzi wa kati watakuwa ni, Bakary Papa Gassama-Gambia na Slim Jedidi-Tunisia, washika vibendera ni Jason Joseph Damdoo-Shelisheli, Angesom Ogbamariam-Eritrea, Bechir Hassani-Misri na Sherif Hassan-Misri. Watatu waliobakia wenyewe watachezesha mpira kwa upande wa wanawake ambapo mwamuzi wa kati watakuwa ni Therese Raissa Neguel-Cameroon huku washika vibendera wakiwa ni Tempa Ndha-Benin na Lidwine Pelagie Rokotozafinoro-Madagascar. Katika michuano hiyo timu kutoka nchi za Gabon, Morocco, Misri na Senegal ndio watakuwa wawakilishi wa Afrika kwa upande wa wanaume wakati kwa upande wanawake Cameroon na Afrika Kusini ndio timu pekee zitakazowakilisha Afrika.

No comments:

Post a Comment