Saturday, April 21, 2012

RIJKAARD KUELEKEA MEXICO.

KOCHA wa zamani wa Barcelona Frank Rijkaard ameripotiwa kuhusishwa na tetesi za kuhamia katika klabu ya Chivas ya nchini Mexico. Rijkaard ambaye ana umri wa miaka 49 kwasasa anakinoa kikosi cha timu ya taifa ya Saudia Arabia lakini kwa mujibu chanzo kimoja kilichopo karibu na klabu hiyo kocha huyo yuko karibu kuhamia Mexico kama wakifikia muafaka katika suala la mshahara. Mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Uholanzi wakati akiinoa Barcelona alifanikiwa kushinda mataji mawili ya Ligi Kuu nchini Hispania na moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya kabla ya kuondoka klabuni hapo mwaka 2008. Baada ya kuiacha Barcelona alienda kuinoa Galatasaray kabla ya kwenda Saudi Arabia mwaka jana ingawa hivi sasa anaonekana kutamani kurejea kunoa vilabu baada ya nchi hiyo kutolewa katika mzunguko wa tatu wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2014 kwa nchi za bara la Asia.

No comments:

Post a Comment