Saturday, April 21, 2012

MESSI KARIBUNI KUITWA BABA.

Messi na mpenzi wake Antonella wakivinjari.
Lionel Messi anahesabika kuwa mchezaji bora kuwahi kutokea katika mchezo wa soka hivi karibuni anaweza kukabiliwa na changamoto nyingine nje ya uwanja kutokana na ripoti zilizozagaa kuwa anaweza kuitwa baba. Habari hizo zilianza kusambaa kwa mara ya kwanza katika radio moja nchini Argentina na toka hapo vyombo mbalimbali vya habari vimekuwa vikitangaza habari hizo kwamba mshambuliaji huyo wa Barcelona anategemea kupata mtoto na rafiki yake wa kike wa siku nyingi aitwae Antonella Roccuzzo. Gazeti moja nchini Argentina liitwalo Diario Uno ambapo linatengenezwa katika mji ambao Messi ametokea liliripoti kuwa walijaribu kuwasiliana na wazazi wa Messi kuthibitisha habari hizo lakini hakuna aliyekuwa habari hiyo lakini pia hawakukataa kuhusiana na tetesi hizo. Messi amekuwa mfungaji anayeongoza kwa mabao mengi katika historia ya klabu ya Barcelona akiwa amefunga mabao 234 mpaka sasa akiwa bado na umri mdogo wa 24 tu. Kocha wake Pep Guardiola amethubutu kumfananisha mchezaji huyo na nyota wa zamani wa mpira wa kikapu kutoka Marekani, Michael Jordan.

No comments:

Post a Comment