Saturday, April 28, 2012

ROONEY-WILBECK NEW YORKE-COLE - FERGIE.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, Sir Alex Ferguson anaamini kuwa washambuliaji wake Wayne Rooney na Danny Welbeck wanaweza kufikia rekodi ya klabu hiyo iliyowekwa na kipindi cha na washambuliaji Dwight Yorke na Andy Cole. Welbeck alifunga bao lake la 12 msimu huu wakati United ilipotoa sare ya mabao 4-4 na Everton wakati Rooney alifunga mawili na mabao 33 msimu huu. Uelewano wa Rooney na Welbeck katika safu ya ushambuliaji wa klabu hiyo kwasasa unarudisha nyuma kumbukumbu ya miaka ya nyuma wakati Yorke na Cole kufunga mabao 53 katika msimu wa 1998-1999 na kuiwezesha timu hiyo kushinda mataji matatu muhimu. Ferguson amesema kuwa kiwango walichokionyesha wachezaji hao kinakaribiana na kipindi cha kina Cole na katika miaka michache ijayo wataweza kufikia huko kwani umri wao bao unaruhusu.

No comments:

Post a Comment