Thursday, April 19, 2012

TIMU YA TAIFA YA SUDANI KUWASILI LEO MCHANA

Timu ya Taifa ya Sudan (U20) inawasili leo saa 7.25 mchana (Aprili 19 mwaka huu) kwa ndege ya Ethiopian Airlines namba ET 805 ikiwa na msafara wa watu 30. Sudan inatarajia kufikia kwenye hoteli ya Rungwe iliyoko eneo la Kariakoo, Dar es Salaam.
Timu hiyo inatarajia kufanya mazoezi leo saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Karume, na kesho itafanya mazoezi Uwanja wa Taifa. Vilevile kesho saa 4 asubuhi kutakuwa na mkutano wa makocha wa Tanzania U20 na Sudan U20 na Waandishi wa Habari ofisi za TFF.

No comments:

Post a Comment