Saturday, April 28, 2012

WATUHUMIWA WA MABOMU SCOTTLAND WAHUKUMIWA MIAKA MITANO.

Neil Lennon
WATU wawili ambao walituma bomu kwenye barua kumwendea meneja wa klabu ya Celtic ya Scottland Neil Lennon wamehukumiwa vifungo vya miaka mitano jela. Watu hao ambao ni Trevor Muirhead na Neil McKenzie mara ya kwanza walikuwa wameshitakiwa na makosa ya kula njama za mauaji, lakini badala yake walihukumiwa na makosa ya kula njama za mashambulizi baada ya kutuma kifaa ambacho waliamini kwamba kingelipuka. Watu hao walituma mabomu hayo mwaka uliopita kwenda kwa Lennon, Mshauri wa Kisheria wa klabu ya Celtic Trish Godman na wakili wa Lennon ambaye ni marehemu anayeitwa Paul McBride. Vifurushi hivyo vya mabomu vilikamatwa kabla ya kuwafikia walengwa waliokusudiwa na havikulipuka.

No comments:

Post a Comment