Saturday, April 28, 2012

BARCELONA YAPATA UDHAMINI KUTOKA THAILAND.

KLABU ya Barcelona imetangaza ratiba yake ya kufanya ziara nchini Thailand mwaka ujao baada ya kusaini mkataba wa udhamini wa miaka mitatu wenye thamani ya euro milioni 12 na Kampuni ya Thai Beverage. Makamu wa Rais wa klabu hiyo, Javier Faus amethibitisha ziara hiyo na kusema kwamba wana nia ya kuongeza mashabiki katika bara ya Asia hususani upande wa Kusini Mashariki mwa bara hilo. Faus amesema kuwa ziara hiyo ina manufaa makubwa kwao kwani hivi sasa wamejikusanyia mashabiki wengi zaidi barani Asia kuliko Ulaya hivyo wanatarajia kuweka mpango wa miaka 10-20 katika ukanda huo. Aliendelea kusema kuwa wamefurahishwa na Thailand kuwa nchi ya kwanza Asia kuwaunga mkono na mkataba walioingia utasaidia mashabiki nchini humo kuielewa klabu hiyo. Naye Meneja Masoko wa kampuni hiyo, Sorrakit Latitham pia alieleza kuwa kampuni yake inajivunia kuandaa ziara ya klabu hiyo ambayo ndio inayohesabika kuwa ni klabu bora zaidi duniani kwa sasa.

No comments:

Post a Comment