Saturday, April 28, 2012

FAINALI YA CHAMPIONS LEAGUE KUONYEHSWA LIVE OLYMPIC STADIUM, MUNICH.

Olympic Stadium, Munich, Germany.
SHIRIKISHO la Soka barani Ulaya-UEFA limesema kuwa Uwanja wa Olimpiki uliopo jijini Munich, Ujerumani utaonyesha mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati Bayern Munich itakapochuana na Chelsea katika Uwanja wa Allianz Arena Mei 19 mwaka huu. Beyern imepata maombi ya tiketi zaidi ya milioni ya mashabiki wakihitaji tiketi katika uwanja wao wa Allianz Arena ambapo klabu hiyo imepewa tiketi 17,000 katika uwanja huo wenye uwezo wa kuingiza mashabiki wapatao 66,000. Mashabiki ambao watakosa tiketi za kushudia mchezo huo sasa wataweza kuona mchezo huo moja kwa moja kupitia luninga katika uwanja wa Olimpiki ambapo tiketi zitakuwa zikiuzwa kwa euro tano moja katika viti 65,000 vilivyopo uwanja huo ambao ulikuwa ukitumiwa na Bayern kabla ya kuhamia Allianz Arena mwaka 2005. Hii ni mara ya kwanza kwa fainali ya Kombe la Klabu Bingwa Ulaya kuonyeshwa rasmi katika luninga uwanjani na tiketi zake kuuzwa katika mtandao.

No comments:

Post a Comment