Sunday, April 29, 2012

ROBINHO AACHWA MILAN.

MSHAMBULIAJI wa AC Milan, Robinho ameachwa katika kikosi cha timu hiyo na kocha Massimiliano Allegri kutokana na kushuka kiwango chake katika siku za karibuni. Akihojiwa Allegri alikiri kuwa mchezaji huyo hayuko katika kiwango chake hivyo ameona ni bra kumpumzisha kwanza. Robinho ambaye ana umri wa miaka 28 amefunga mabao matano tu mpaka sasa katika michezo 26 alizocheza rekodi ambayo imemkera Allegri akidai kuwa hapendi kuwa na mchezaji ambaye msimu mzima anacheza chini ya kiwango. Kocha huyo pia akasirishwa na kiwango cha kiungo mkongwe kutoka Uholanzi Clarence Seedorf ingawa kumuacha kwake kwenye kikosi hicho ambacho kitachuana na Siena ni kutokana na majeruhi yanayomsumbua. Kinara wa mabao Zlatan Ibrahimovic ambaye ana mabao 24 msimu huu anatarajiwa kuanza kucheza katika kikosi hicho pamoja na Antonio Cassano au Stephan El-Shaarawy wakisaidiwa na Kevin-Prince Boateng. Milan inashika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu nchini Italia wakiwa nyuma kwa alama tatu kwa vinara wa ligi hiyo Juventus huku wakiwa wamebakiwa na michezo minne kabla msimu kumalizika.

No comments:

Post a Comment