Sunday, April 29, 2012

WENGER AKERWA NA VITENDO VYA UNYANYASAJI KUTOKA KWA MASHABIKI.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amesema kuwa kuna kubwa ya kufanya ili kudhibiti vitendo vya unyanyasaji kutoka kwa mashabiki. Kauli ya kocha huyo imekuja baada ya baadhi ya mashabiki wa timu ya Stoke City kutoa kauli za matusi wakati wa mchezo baina ya timu hizo ambao walitoka sare ya bao 1-1 katika Uwanja wa Britannia. Wenger amesema kuwa anafikiri siku moja mchezo wa mpira wa miguu unaweza kuachana na mambo hayo kwani soka ni mchezo wa burudani na sio uadui kama baadhi ya mashabiki wanavyofikiri. Upinzani kati ya timu ya Arsenal na Stoke ulikuwa zaidi katika kipindi karibuni ambapo pia walikuwa wakimzomea kiungo wa Arsenal Aaron Ramsey atika mchezo huo. Mashabiki wa Stoke kumzomea Ramsey kunakuwa kama ni kulipiza kisasi baada ya kiungo huyo kuvunjika mguu baada ya kuchezewa vibaya na Ryan Showcross Februari mwaka 2010 katika mchezo baina ya timu hizo ambapo toka kipindi hicho beki huyo wa Stoke amekuwa akizomewa na baadhi ya mashabiki wa Arsenal.

No comments:

Post a Comment