Sunday, April 29, 2012

BALOTELLI CAN BE TRUSTED - MANCINI.

MENEJA wa Manchester City, Roberto Mancini amesema kuwa atamwamini mshambuliaji wake Mario Balotelli kama atamchezesha katika mchezo dhidi ya mahasimu wao Manchester United. Katika mkutano na waandishi wa habari wiki nne zilizopita Mancini alinukuliwa akisema kuwa hawezi kumwani mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Italia kwakuwa haeleweki. Balotelli mwenye umri wa miaka 21 hajacheza mechi toka alipotolewa kwa kadi nyekundu katika mchezo dhidi ya Arsenal mapema mwezi huu ambapo katika kipindi hicho Mancini alisema kuwa hawezi kuchezesha tena mshambuliaji huyo msimu huu. Mancini amesema kuwa baada ya mchezaji huyo kuomba msamaha kutokana na tukio alilofanya anaweza kumpa nafasi ya kucheza katika mchezo huo kwakuwa amekuwa akifanya vyema kwenye mazoezi na wenzake wa kikosi cha kwanza. Balotelli alitolewa katika Uwanja wa Emirates baada ya kuchezea vibaya Bacary Sagna na kupewa kadi ya pili ya njano ambapo City walifungwa bao 1-0 na Arsenal.

No comments:

Post a Comment