Sunday, April 29, 2012

FENERBAHCE YAJITOA KUMWANIA DIARRA.

KLABU ya Fenerbahce ya Uturuki imejitoa katika mbio za kumwania kiungo wa klabu ya Real Madrid ya Hispania Lassana Diarra. Klabu hiyo inayotoka jijini Istanbul ilikuwa ikimhitaji kiungo huyo wa zamani wa Arsenal ili kuongeza nguvu katika safu ya kiungo ya klabu hiyo lakini kutokana matatizo ya kifedha yanayoikabili klabu hiyo imeshindwa kuendelea na mbio zake na kumchukua. Diarra hivi sasa amekuwa ziada ya mahitaji ya klabu ya Madrid ambapo hivi sasa klabu hiyo ipo tayari kupokea pesa kutoka timu yoyote kama watamuhitaji mchezaji huyo. Kiungo huyo ambaye pia ameshawahi kuichezea klabu ya Chelsea pia anahusishwa na kuhitajika katika klabu ya Galatasaray ambapo taarifa zinasema kwamba wako katika mazungumzo.

No comments:

Post a Comment