Tuesday, May 1, 2012

REDKNAPP AMKUBALI HODGSON KUINOA UINGEREZA.

MENEJA wa Tottenham Hotspurs, Harry Redknapp amesema kuwa haoni tatizo mpinzani wake Roy Hodgson kupewa kibarua cha kukinoa kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza. Redknapp amekuwa akitajwa kukinoa kikosi hicho toka aliyekuwa kocha wa timu hiyo Fabio Capello alipojiuzulu wadhifa huo Februari ambapo Chama cha Soka cha Uingereza-FA kimeamua kuanza mazungumzo ya awali na Hodgson ambaye ni kocha West Bromwich Albion. Hodgson ambaye ana miaka 64 amewahi kushinda mataji nane ya ligi katika nchi mbili tofauti akiwa anafundisha vilabu vitatu tofauti ambapo pia amewahi kuzifundisha timu za Switzerland, Finland na Umoja wa Falme za Kiarabu-UAE. Kocha huyo alikutana na viongozi wa FA jana katika mkutano uliochukua muda wa saa nne uliofanyika katika Uwanja wa Wembley jijini London. Redknapp amesema kuwa kwasasa anafurahishwa na kibarua chake katika klabu ya Tottenham na anamtakia mafanikio Hodgson kama atapewa kibarua cha kionoa timu hiyo kwani anaamini anaiweza kazi hiyo kutokana na uzoefu mkubwa aliokuwa nao katika soka ya kimataifa. FA inatarajiwa kumtangaza Hodgson kama kocha mpya wa timu ya taifa ya nchi hiyo baadae leo mbele ya vyombo vya habari.

No comments:

Post a Comment