Thursday, May 31, 2012

STARS YAONDOKA BILA BOBAN NA CHOLLO.

Wachezaji wa Kilimanjaro Taifa Stars wameondoka Dsm alfajiri ya leo tayari kwa mchezo wao dhidi ya Ivory Coast utakoachezwa jumamosi huko ABIJAN
Kocha mkuu wa timu hiyo KIM PAULSEN amewataja wachezaji hao wawili zaidi kuwa ni HARUNA MOSH BOBAN na Saidi nassoro chollo ambao ni majeruhi wapya. Wachezaji ambao walikuwa ni majeruhi wakiwa kambini ni NURDIN BAKAR na THOMAS ULIMWENGU. Wakiwa katika uwanja wa Jomo Kenyatta , wachezaji wa TAIFA STARS ilibidi wakae kwa muda wa saa tano kusubiri ndege inayokwenda Ivory coast baada ya ile ya mwanzo muda wake kubadilihwa. Kutokana na kuchelewa huko huenda kikosi cha TAIFA STARS kilichtarajia kuingia IVORY COAST saa nane mchana kwa saa za Afrika mashariki sasa itaingia kati ya Saa mbili au tatu kwa saa za afrika mashariki.

No comments:

Post a Comment