Saturday, June 30, 2012

BOLT ACHEMSHA MBELE YA BLAKE.

MWANARIADHA nyota wa mbio fupi wa Jamaica Usain Bolt ameshindwa kutamba katika fainali ya mbio za taifa za nchi hiyo baada ya kushika nafasi ya pili akitumia muda wa sekunde 9.86. Nafasi ya kwanza katika mbio hizo ilishikiliwa na Yohane Blake ambaye alitumia muda wa sekunde 9.75 na kuipiku rekodi ya Bolt aliyoweka mwaka huu ya sekunde 9.76 katika mashindano yaliyofanyika jijini Rome, Italia mwezi uliopita. Katika mbio hizo Bolt alianza taratibu mwisho lakini alijitutumua karibu mwishoni wa mbio hizo na kujikuta akimaliza mbele ya Asafa Powell ambaye alishika nafasi ya tatu akitumia muda wa sekunde 9.88. Akihojiwa mara baada yam bio hizo Bolt alikiri kuwa alipata tatizo katika kuanza lakini alipuuzia na kujipa moyo kwamba hatakiwi kukata tamaa ndio maana akafanikiwa kukamata nafasi ya pili imemuwezesha kufuzu michuano ya Olimpiki itakayofanyika jijini London mwaka huu. Hii ni mara ya kwanza Bolt kushindwa mbio za nchini kwake toka mwaka 2004 alipojiunga rasmi na mbio za kulipwa ambapo pia ni bingwa mtetezi wa mbio za mita 200 katika michuano olimpiki.

No comments:

Post a Comment