Friday, June 29, 2012

VALCKE ARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA WORLD CUP NCHINI BRAZIL.

Jerome Valcke.

KATIBU Mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Jerome Valcke amesema kuwa Brazil inaendelea vizuri na maandalizi ya michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2014 baada ya kufaya ziara ya siku tatu nchini humo kukagua maendeleo ya maandalizi hayo. Valcke alitembelea miji ya Racife, Natal na Brasilia mbayo itakuwa wenyeji wa michuano pamoja na kuzungumza na wajumbe wa kamati ya maandalizi ambao walimpa taarifa ya hatua walizofikia katika maandalizi ya Kombe la Dunia na Kombe la shirikisho ambalo litachezwa mwaka kesho. Valcke amesema kuwa miradi mingi inaenda vizuri kila mtu anafanya kazi kwa bidii kuhakikisha wanaandaa michuano iliyo bora. FIFA pia ilitangaza kuwa ratiba ya Kombe la Dunia itapangwa katika mji wa Costa do Sauipe ambao uko Kaskazini-Mashariki mwa nchi hiyo Desemba mwaka 2013 wakati ratiba ya michuano ya Confederation itapangwa Desemba mwaka huu jijini Sao Paulo.

No comments:

Post a Comment