Friday, June 29, 2012

ITALIA YAKATA TIKETI CONFEDERATION CUP BAADA YA KUIADHIRI UJERUMANI.


 

TIMU ya taifa ya Italia imekata tiketi ya kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho litakalofanyika mwakani nchini Brazil baada ya kufanikiwa kuingia fainali ya michuano ya Ulaya kwa kuifunga Ujerumani mabao 2-1 jijini Warsaw, Poland. Hispania pia wamefuzu hatua ya fainali ambayo itachezwa Jumapili jijini Kiev, Ukraine lakini wenyewe walikuwa wamefuzu moja kwa moja michuano ya shirikisho kwakuwa wenyewe ndio mabingwa wa dunia kwa sasa hivyo Italia ndio watakaowakilisha Ulaya kwenye michuano hiyo. Katika michuano hiyo Spanish na Italia zitawakilishwa bara la Ulaya wakati Japan ikiwakilisha bara la Asia kwakuwa ndio mabingwa wa bara hilo huku Mexico na Uruguay zikiwakilisha bara la Amerika Kusini na CONCACAF na Brazil wenyewe watakuwepo kama wenyeji wa michuano hiyo. Nchi ya Tahiti nayo imefuzu baada ya kuwa mabingwa wa Oceania wakati mwakilishi wa Afrika atapatikana katika michuano ya Mataifa ya Afrika yatakayofanyika mapema mwakani. Michuano ya Kombe la Shirikisho inatarajiwa kuanza kutimua vumbi June 15 mpaka 30 mwakani ambapo michezo ya ufunguzi itafanyika jijini Brasilia nusu fainali itachezwa katika miji ya Belo Horizonte na Fortaleza wakati fainali itapigwa katika jiji la Rio de Janeiro.

No comments:

Post a Comment