Tuesday, July 31, 2012

ALMUNIA ATIMKIA WATFORD.

Emmanuel Almunia.
KLABU ya Arsenal imesema kuwakipa wake wa zamani Manuel Almunia amejiunga na klabu ya Watford inayoshiriki ligi daraja pili nchini Uingereza. Almunia ambaye amepewa mkataba wa mwaka mmoja anakuwa mmoja kati ya wachezaji wapya saba waliosajiliwa na Watford ambayo inanolewa na kocha Gianfranco Zola. Taarifa iliyotumwa katika mtandao wa klabu ya Arsenal ilithibitisha kuwa ni kweli klabu hiyo imemwachia Almunia kwenda Watford kwa mkataba wa mwaka mmoja. Almunia amecheza michezo 175 akiwa na klabu ya Arsenal ukiwemo mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 2006 dhidi ya Barcelona ambao aliingia kama mchezaji wa akiba lakini alipoteza namba katika kikosi cha kwanza cha klabu hiyo kwa Wojciech Szczesny ambaye ni raia wa Poland. Watford ambayo katika siku za karibuni ilinunuliwa na familia ya Pozzo ambao pia wanamiliki klabu ya Udinese inayoshiriki Ligi Kuu nchini Italia na Granada ya Hispania, pia imewasajili Fitz Hall, Almen Abdi, Matej Vydra na Steve Leo Beleck.

No comments:

Post a Comment