Tuesday, July 31, 2012

MORGANELLA ATIMULIWA KAMBINI.

Michel Morganella.
BEKI wa kimataifa wa Switzerland, Michel Morganella ameondolewa katika kikosi cha timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 23 inayoshiriki michuano ya Olimpiki jijini London baada ya kutuma ujumbe wa kibaguzi katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter kwenda kwa mchezaji wa Korea Kusini. Viongozi wa timu hiyo walimuondoa mchezaji huyo katika kikosi hicho baada ya kutuma ujumbe huo kufuatia kufungwa na Korea Kusini kwa mabao 2-1 Jumapili iliyopita. Mkuu wa msafara wa nchi hiyo kwenye michuano ya olimpiki Gian Gilli amesema kuwa beki huyo ametuma ujumbe ambao unadhalilisha kwa watu wa Korea Kusini pamoja na timu yao ya taifa hivyo baada ya kupata ushauri kutoka kwa Chama Cha Soka cha Switzerland wakaamua kumuondoa kikosini mchezaji huyo. Mchezaji huyo alikubali maamuzi yaliyochukuliwa na kuomba radhi kutokana na tabia aliyoionyesha ingawa alijitetea kuwa zilikuwa ni hasira baada ya kupoteza mchezo dhidi ya timu hiyo.

No comments:

Post a Comment