Friday, July 27, 2012

BOLT YUKO FITI KUTETEA TAJI LAKE.

Usain Bolt.
MWANARIADHA nyota wa mbio fupi kutoka Jamaica, Usain Bolt amekiri kuwa maumivu ambayo yalikuwa yakimsumbua yaliathiri kiwango chake kwa kiasi fulani. Bolt amesema kuwa maumivu hayo ya mgongo kwasasa yamepona na yuko tayari kutetea taji lake wakati atakapopeperusha bendera ya nchi yake katika sherehe za ufunguzi wa michuano hiyo baadae leo. Nyota huyo ambaye anashikilia rekodi ya dunia ya sekunde 9.58 katika mbio za mita 100 alishindwa kutamba mbele ya mjamaica mwenzake Yohan Blake katika mbio za majaribio zilizofanyika jijini Kingston na baadae kukosa mbio za Diamond League zilizofanyika jijini Monaco. Akihojiwa Bolt amesema kuwa katika mbio hizo alikuwa yuko sawa lakini hakuwa katika kiwango chake ambacho amekizoea lakini anashukuru baada ya mapumziko na mazoezi aliyokuwa akifanya anaamini anaweza kutete taji lake kwenye michuano hiyo. Bolt pia alishukuru kwa kupewa heshima ya kubeba bendera ya nchi yake katika sherehe za ufunguzi wa michuano hiyo ambayo inatarajiwa kufanyika baadae usiku.

No comments:

Post a Comment