Friday, July 27, 2012

FA PISSED ME OFF - CAPELLO.

Fabio Capello.

KOCHA mpya wa timu ya taifa ya Italia, Fabio Capello amekituhumu Chama cha Soka cha Uingereza-FA kuvunja mkataba wake kwa kumvua unahodha wa timu ya taifa ya nchi hiyo John Terry. Capello ambaye ni raia wa Italia amesema wakati akitambulishwa kama kocha mpya wa URUSI kuwa kitendo hicho kilimuudhi sana ndio maana akaamua kuachia ngazi. Kocha huyo alichia ngazi Februari mwaka huu baada ya Terry kuvuliwa unahodha wa kikosi hicho kutokana na kukabiliwa na kesi juu ya tuhuma za ubaguzi kwa mchezaji wa Queens Park Rangers, Anton Ferdinand. Kufuatia kauli hiyo ya Capello, FA ilijibu na kusisitiza kuwa walikuwa na mamlaka ya kumvua unahodha Terry. Capello ambaye mkataba wake mpya utamuwezesha kulipwa kiasi cha paundi milioni 7.8 kwa mwaka alikataa kuongelea kwa undani kuhusu Uingereza kutokana na makubaliano yake na FA.

No comments:

Post a Comment