Monday, July 30, 2012

HISPANIA WAAGA MAPEMA MICHUANO YA OLIMPIKI.

TIMU ya taifa ya vijana chini ya miaka 23 ya Hispania imeenguliwa mapema katika michuano ya Olimpiki inayofanyika jijini London baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Honduras ikiwa ni kipigo cha pili mfululizo kufuatia kile walichopata kutoka kwa Japan kwa idadi kama hiyo ya mabao. Honduras ambao walishinda bao la mapema kupitia kwa mshambuliaji wake Jerry Bengtson wamefanikiwa kutinga hatua ya robo fainali pamoja na Japan ambao waliwafunga Morocco bao 1-0 katika kundi D. Katika michezo ya kundi C Brazil ilifanikiwa kusonga mbele baada ya kuifunga Belarus mabao 3-1 wakati Misri ilitoa sare ya bao 1-1 na New Zealand hivyo itabidi washinde mchezo wao wa mwisho dhidi ya Belarus ili waweze kusonga mbele. Mexico ilifanikiwa kushinda mabao 2-0 dhidi ya Gabon katika kundi B wakati Korea Kusini walifanikiwa kushinda mabao 2-1 hivyo kupelekea timu hizo kuwa na alama sawa katika kundi hilo.

No comments:

Post a Comment