Monday, July 30, 2012

HAMILTON AIBUKA KINARA WA MBIO ZA LANGALANGA ZA HUNGARY GRAND PRIX.

DEREVA wa magari yaendayo kasi ya Langalanga kutoka timu ya McLaren, Lewis Hamilton amefanikiwa kushinda mbio za Hungary Grand Prix jana. Hamilton ambaye ni raia wa Uingereza alimaliza mbio hizo kwa kasi zaidi ya wenzake ambao aliwaacha kwa sekunde 0.413 na kufuatiwa na dereva wa timu ya Lotus, Romain Grosjean aliyeshika nafasi ya pili katika mbio hizo. Sebastian Vettel wa timu ya Red Bull alimaliza katika nafasi ya tatu akifutiwa na Jenson Button ambaye ni muingereza kutoka timu ya McLaren pia alimaliza katika nafasi ya nne. Wengine ni Kimi Raikkonen aliyemaliza katika nafasi ya tano akifuatiwa na Fernando Alonso wa timu ya Ferrari katika nafasi ya sita wakati mkali mwingine wa mbio hizo Mark Webber alimaliza katika ya 11. Magari ya Ferrari ambayo yalitamba kipindi cha mvua katika michuano ya Ujerumani katika mbio hizo za majira ya kiangazi yameshindwa na kusababisha kupunguza pengo la alama ambazo Alonso alikuwa akiongoza katika orodha ya madereva bora duniani.

No comments:

Post a Comment