Monday, July 30, 2012

WILSHERE KUREJEA UWANJANI OCTOBA.

Jack Wilshere.
MENEJA wa klabu ya Arsenal Arsenal Wenger amesema kuwa kiungo nyota wa klabu hiyo Jack Wilshere hata kuwa sehemu ya kikosi chake katika michezo ya mwanzo wa Ligi Kuu nchini Uingereza kutokana na majeraha yanamsumbua. Wilshere ambaye ana miaka 20 alishindwa kucheza msimu uliopita kutokana na kufanyiwa upasuaji wa goti aliofanyiwa Mei mwaka jana. Wenger ambaye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kukamilisha ziara ya bara la Asia jijini Hong Kong amesema kuwa anatarajia mchezaji huyo kurejea dimbani mwezi Octoba. Wakati akiuguza goti lake Wilshere alilitonesha tena wakati akifanya mazoezi ili arejee uwanjani na hivyo kumfanya mchezaji kukosa michuano ya Ulaya iliyomalizika Julai mosi mwaka huu ambapo anatarajiwa kuanza mazoezi mepesi Agosti na akitarajia kurejea uwanjani Octoba.

No comments:

Post a Comment