Sunday, July 29, 2012

YE SHIWEN AWEKA REKODI YA DUNIA OLIMPIKI.

Ye Shiwen.
MUOGELEAJI Ye Shiwen kutoka China amevunja rekodi ya dunia ya mita 400 katika mchezo huo na kunyakuwa medali ya dhahabu katika michuano ya Olimpiki inayoendelea jijini London, Uingereza. Shiwen mwenye miaka 16 aliweka rekodi hiyo akitumia muda bora wa dakika 4:28:43 mbele ya bingwa wa dunia kutoka Marekani Elizabeth Beisel na Li Xuanxu ambaye pia anatoka China. Muogeleaji huyo alivunja rekodi ya muda wa dakika 4:29:45 ambayo ilikuwa imewekwa na Stephanie Rice kutoka Australia katika michuano ya olimpiki iliyofanyika Beijing mwaka 2008. Muogeleaji kutoka Uingereza Hannah Miley ambaye alishinda medali ya fedha katika mashindano ya dunia mwaka jana na kutegemewa kufanya vizuri katika mashindano hayo alishindwa kutamba baada ya kumaliza katika nafasi ya tano. Mara baada ya mashindano hayo Miley aliomba radhi mashabiki wake ambao walitarajia atafanya vizuri ambapo kwasasa amesema anahamishia nguvu zake katika mbio za kuogelea za mita 200 kuhakikisha anafanya vyema.

No comments:

Post a Comment