Sunday, July 29, 2012

FEDERER, SERENA WAANZA VYEMA OLIMPIKI.

Roger Federer.
WACHEZA tenisi nyota Roger Federer na Serena Williams wameanza vyema kampeni zao za kuhakikisha wanaondoka na medali ya dhahabu katika michuano ya Olimpiki baada ya kushinda michezo yao ya kwanza. Federer kutoka Switzerland ambaye anashikilia namba moja katika orodha za ubora za mchezo huo duniani kwa upande wa wanaume alifanikiwa kumfunga Alejandro Falla kutoka Colombia kwa 6-3 5-7 6-3. Kwa upande wa wanawake Williams ambaye anashika nafasi ya nne katika orodha za ubora alifanikiwa kumfunga kirahisi Jelena Jankovic kutoka Serbia kwa 6-3 6-1 na kufanikiwa kutinga raundi ya pili. Kim Clijsters kutoka Ubelgiji ambaye amepanga kustaafu mchezo huo mwishoni mwa mwaka huu alifanikiwa kumfunga Roberta Vinci kutoka Italia kwa 6-1 6-4 ambapo sasa anatarajiwa kukutana na Carla Suarez wa Hispania katika mzunguko wa pili wakati Serena atakutana na Urszula Radwanska wa Poland. Federer atacheza na Julien Benneteau kutoka Ufaransa ambaye alimfunga kwa seti tano katika michuano ya Wembledon iliyopita.

No comments:

Post a Comment