Sunday, August 26, 2012

ABBAS AMKINGIA KIFUA KOCHA MPYA ZAMALEK.

MWENYEKITI wa klabu ya Zamalek ya Misri, Mamdouh Abbas amesema kuwa hawana mpango wa kumtimua kocha wa klabu hiyo Jovran Vieira pamoja na matokeo mabovu waliyopata katika kipindi cha karibuni na kupelekea kuengiliwa katika Ligi ya mabingwa Afrika. Akihojiwa Abbas pia alikataa tetesi kuwa ameanza mazungumzo na mapacha Hossam na Ibrahim Hassan ili kuziba pengo na Vieira ambaye ni raia wa Brazil. Abbas amesema kuwa umepita mwezi mmoja toka wamwajiri Vieira hivyo hawana sababu ya kumfukuza kwasababu wanaamini uwezo wake na ataipeleka klabu hiyo mbali. Hossam na Ibrahim waliwahi kuinoa Zamalek katika msimu wa mwaka 2010-2011 kabla ya bodi ya klabu hiyo kuwatimua na kumwajiri Hassan Shehata ambaye aliondoka mwezi uliopita.

No comments:

Post a Comment