Sunday, August 26, 2012

LIVERPOOL YAMNASA SAHIN KWA MKOPO.

KLABU ya Liverpool ya nchini Uingereza imefanikiwa kumsajili kwa mkopo kiungo Nuri Sahin kutoka klabu ya Real Madrid ya nchini Hispania. Kiungo huyo wa kimataifa wa Uturuki ambaye ana umri wa miaka 23 anakuwa mchezaji wan ne kusajiliwa katika kikosi hicho ambacho kinanolewa na Brendan Rodgers ambaye pia amewasajili Joe Allen, Fabio Borin na Oussama Assaidi. Sahin ambaye pia alikuwa akiwindwa na klabu ya Arsenal amesema kuwa kiungo wa zamani wa klabu hiyo ambaye sasa anacheza Madrid Xabi Alonso ndiye aliyemshauri aende kujiunga na klabu hiyo. Akihojiwa mara baada ya kutua Anfield, Sahin amesema amekwenda katika klabu hiyo ili kuisaidia kushinda vikombe na kurejesha makali yake kama ilivyokuwa zamani. Mbali na ushauri aliopewa na Alonso lakini pia mchezaji huyo alishauriwa na kocha wa Madrid Jose Mourinho kuwa Ligi Kuu nchini Uingereza itakuwa nzuri kwake kukuza kiwango chake.

No comments:

Post a Comment