Sunday, August 26, 2012

GALATASARAY YAJITOA MBIO ZA KUMWANIA KAKA.

RAIS wa klabu ya Galatasaray ya nchini Uturuki, Unal Aysal ameondoa uwezekano wa kumsajili kiungo wa klabu ya Real Madrid Kaka. Aysal mwenye umri wa miaka 71 mapema alidai kuwa klabu yake hiyo ambao ndio mabingwa wa Ligi Kuu nchini Uturuki inaweza kumsajili nyota huyo ambaye pia amewahi kukipiga katika klabu ya AC Milan ya Italia. Kaka ambaye ni raia wa Brazil amekuwa akihusishwa na suala la kuondoka katika kipindi hiki cha majira ya kiangazi na kocha wa Madrid Jose Mourinho hakumjumuisha mchezaji huyo katika mchezo dhidi ya Barcelona uliochezwa katikati ya wiki iliyopita na Getafe ambao utachezwa baadae leo. Rais huyo amesema kuwa alizungumza na kocha wa klabu hiyo Fatih Terim na kumfahamisha kuwa kama anahitaji kuongeza katika kikosi hicho basi inabidi aongeze beki na sio Kaka ambaye anacheza nafasi ya kiungo mshambuliaji. Galatasaray inakabiliwa na mchezo mgumu wa mahasimu wao wa jijini Istabul timu ya Besiktas ambao unatarajiwa kupigwa baadae leo.

No comments:

Post a Comment