Sunday, August 26, 2012

BOLT NDANI YA OLD TRAFORD.

MWANARIADHA nyota wa mbio fupi kutoka Jamaica, Usain Bolt alikuwa mgeni rasmi katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza kati Manchester United na Fulham uliochezwa katika Uwanja wa old Traford. 
Bolt ambaye ana medali sita za dhahabu za olimpiki ni mshabiki wa United kwa kipindi kirefu na katika siku za karibuni alikaririwa akisema kuwa anataka kuwa mchezaji wa klabu hiyo. Nyota huyo wa mbio fupi alitambulishwa mbele ya mashabiki waliohudhuria mchezo huo ambao walikuwa wakipiga kelele ya kumtaka Ferguson amsajili mwanaridha huyo ili kuimarisha safu yake ya ushambuliaji. 
Mshambuliaji mpya wa klabu hiyo Robin van Persie na mkongwe Ryan Giggs walipata nafasi ya kupiga picha ya pamoja na Bolt kabla ya kuanza kwa mchezo huo ambao United ilishinda kwa mabao 3-2.

No comments:

Post a Comment