Friday, August 24, 2012

BOLT, BLAKE WANG'ARA DIAMOND LEAGUE.

MKIMBIAJI nyota wa mbio fupi kutoka Jamaica, Yohane Blake amefanikiwa kuweka rekodi katika mbio za mita 100 na kuwa mtu wa tatu mwenye kasi zaidi huku mjamaica mwenzake Usain Bolt naye akishinda kirahisi mbio za mita 200 katika michuano ya Diamond League iliyofanyika jijini Lausanne. Blake ambaye alishinda medali ya fedha katika mbio za mita 100 na 200 katika michuano ya Olimpiki iliyofanyika jijini London, katika mbio hizo alitumia muda wa sekunde 9.69 Ni Bolt pekee ambaye alinyakuwa medali ya dhahabu katika mbi za mita 100, 200 na 400 kupokezana vijiti, ndio mwenye rekodi ya kukimbia kwa kasi zaidi katika mbio fupi. Akihojiwa mara baada ya mbio hizo Blake amesema kuwa amefurahishwa na muda aliotumia na ana mategemeo ya kufanya vizuri zaidi katika siku zijazo kama ataepuka majeruhi.

No comments:

Post a Comment