Friday, August 24, 2012

MTANANGE WA AL AHLY NA ZAMALEK KUPIGWA SEPTEMBA 16.

SHIRIKISHO la Soka barani Afrika-CAF limepanga mchezo wa mzunguko wa mwisho wa michuano ya Klabu Bingwa Afrika kati ya timu ya Al Ahly na Zamalek ambao ni mahasimu kuchezwa Septemba 16 mwaka huu. Mkurugenzi wa Al Ahly Sayed Abd Al Hafez alithibisha kuwa wamepokea taarifa hizo kutoka CAF ambapo pia mchezo kati TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC na Chelsea Berekum ya Ghana nao utapigwa tarehe kama hiyo na muda mmoja. Mchezo wa klabu hizo kongwe na mahasimu nchini unatarajiwa kupigwa katika Uwanja wa Kijeshi na bila ya uwepo wa mashabiki. Al Hafez amesema kuwa ameamua kusafiri mapema kuelekea nchii DRC kutafuta hoteli nzuri na sehemu ya kufanyia mazoezi kwa ajili ya timu yake wakati itakaposafiri kwenda kucheza na Mazembe ili kuepuka adha waliyopata wakati walikwenda Ghana kucheza na Chelsea. Al Ahly ndio wanaoongoza kundi B wakiwa na alama 10 baada ya kushinda michezo mitatu na kutoa sare mmoja na sasa watakwenda Lubumbashi kwa ajili ya mchezo dhidi ya Mazembe utakaochezwa Septemba 2 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment