Friday, August 24, 2012

UWANJA WA BOMBONERA WAFUNGIWA KWA VURUGU.

MAOFISA wa usalama wa Serikali nchini Argentina wameufungia uwanja wa Boca Juniors ikiwa kama adhabu kwa vurugu zilizofanywa na mashabiki wa klabu hiyo baada ya kumalizika kwa mchezo wa Klabu Bingwa ya Amerika Kusini maarufu kama Copa Sudamericana dhidi ya Independiente. Ofisa Mkuu wa Usalama nchini humo Dario Ruiz amesema kuwa uwanja huo unatumiwa na Boca ambao unaitwa Bombonera utafungiwa kuchezewa mchezo wa Ligi Kuu nchini humo. Vurugu zilitokea baada ya Independiente kusawazisha bao kwa penati ya dakika za mwisho na kupelekea timu hizo kutoka sare ya mabao 3-3 ambapo mashabiki waliokuwa wamekaa karibu na benchi la Independiente walivunja uzio uliokuwepo na kuingia uwanjani. Msemaji wa Boca amesema katika taarifa yao waliyotuma katika mtandao kuwa wameshawagundua mashabiki wanne waliohusika na vurugu hizo na wanatarajia kuwafungia kuingia katika uwanja huo. Vurugu zimekuwa tishio katika mechi nyingi za soka nchini Argentina kutokana na vikundi vya wahuni kutawala katika maeneo ya karibu na viwanja nchini humo.

No comments:

Post a Comment