Tuesday, August 28, 2012

FERGUSON AWAZUIA MAKINDA WAKE KUENDESHA MAGARI YA KIFAHARI.


MENEJA wa klabu ya Manchester United, Sir Alex Ferguson amewazuia wachezaji wake nyota wenye umri mdogo kuendesha magari ya kifahari ya kimichezo ya Chevrolet ambao ndio watakuwa wadhamini wao wapya. United imetiliana saini ya mamilioni paundi na kampuni kongwe ya magari ya nchini Marekani ambao jina lao litaonekana katika jezi za klabu hiyo mwanzoni mwa msimu wa mwaka 2014-2015. Kutokana na mkataba huo, kampuni hiyo ilitoa ofa kwa wachezaji wa kikosi cha kwanza cha United kuchagua gari lolote la kifahari ambalo linatengenezwa na kampuni hiyo.  
Aina ya magari ya Chevrolet.
Hatahivyo kuna tetesi kuwa Ferguson aliingilia suala hilo kati na kudai kuwa wachezaji wote wenye umri wa miaka chini 23 hata kama atakuwepo katika kikosi cha kwanza hataruhusiwa kutoa oda ya kueletewa gari la kampuni hiyo. Hiyo itamaanisha kuwa mshambuliaji Danny Welbeck mwenye umri wa miaka 21, mabeki Phil Jones mwenye umri wa miaka 20, Chris Smalling miaka 22 na Rafael miaka 22 pia hawataruhusiwa kuendesha gari aina yoyote mpaka waruhusiwe na Ferguson. Hatua ya Ferguson imekuja ili kuwadhibiti wachezaji hao makinda wasijione kama tayari wamekuwa mastaa na kushindwa kucheza soka kwa kiwango cha juu.

No comments:

Post a Comment