Tuesday, August 28, 2012

FA KUITOSA UMBRO NA KUINGIA MKATABA MPYA NA NIKE.

KAMPUNI kongwe ya vifaa vya michezo ya Marekani, Nike iko mbioni kusaini mkataba wa kuisambazia vifaa vya michezo timu ya taifa ya Uingereza. Nike inatarajia kuanza kuisambazia timu hiyo jezi mpya za kuchezea ugenini mapema mwaka ujao pamoja na ukweli kwamba mkataba wa timu hiyo na kampuni ya Umbro unatarajiwa kuisha mwaka 2018. Mkataba huo ambao utakiwezesha Chama cha Soka cha Uingereza-FA kuvuna mamilioni ya paundi, utaonekana kama mashindano kati ya kampuni hizo baada ya mahasimu wao wakubwa kampuni ya Adidas ya Ujerumani kutamba katika michuano ya olimpiki kwa kusambaza vifaa kwa timu ya kombaini ya Uingereza iliyoshiriki michuano hiyo. Wiki iliyopita maofisa wa FA walikuwa tayari kutangaza kuwa mkataba wao na Umbro kampuni ambayo ina maskani katika jiji la Manchester unaweza kuvunjika lakini maofisa hao waliacha kufanya hivyo mpaka watapokamilisha suala la mkataba mpya na Nike.

No comments:

Post a Comment