Tuesday, August 21, 2012

KLABU YA MACEDONIA YAFUNGIWA MIAKA MINNE BAADA YA WACHEZAJI KUPIMWA NA KUKUTWA POSITIVE NA MADAWA YALIYOKATAZWA MICHEZONI.

SHIRIKISHO la Soka barani Ulaya-UEFA limeifungia klabu ya Rabotnicki ya Macedonia miaka minne kushiriki michuano inayoandaliwa na bara hilo baada ya wachezaji wake wawili kupimwa na kukutwa wametumia madawa yaliyokatazwa michezoni. Klabu hiyo pia imetozwa faini ya euro 30,000 baada ya wachezaji hao Milovan Petrovic na Dino Najdoski kukutwa wakiwa wametumia dawa hizo zilizokatazwa kufuatia kipigo cha mabao 6-0 walichopata kutoka kwa Lazio ya Italia katika mchezo wa mtoano wa michuano ya Ligi ya Ulaya maarufu kama Europa League. Mbali na kufungiwa kwa klabu hiyo, wachezaji hao pia walifungiwa mwaka mmoja kila mmoja wakati daktari wa timu hiyo Mihajlo Ivanovski na mwalimu wa viungo Darko Velcevski nao walifungiwa kujishughulisha na masuala ya michezo kwa kipindi cha miaka mitatu kila mmoja. Mbali na adhabu hizo UEFA pia imetuma maombi Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kuidhinisha adhabu hiyo ili wasiweze kushiriki mashindano yoyote duniani.

No comments:

Post a Comment