Tuesday, August 21, 2012

ADEBAYOR AKUBALI KUKATWA MSHAHARA ILI AENDE MOJA KWA MOJA CITY.

MSHAMBULIAJI nyota wa Manchester City ambaye anacheza kwa mkopo katika klabu ya Tottenham Hotspurs anatarajiwa kukamilisha mkataba wake wa moja kwa moja kuhamia klabu hiyo yenye maskani yake jijini London. City na Spurs tayari zilishafikia makubaliano ya kuuziana mchezaji huyo kwa ada ya paundi milioni tano wiki sita zilizopita lakini uhamisho huo ulikwamishwa kutokana na kushindwa kufikia maelewano ya mambo binafsi ya mchezaji huyo na klabu hiyo. Lakini hatimaye mchezaji huyo amekubali kukatwa kiasi kikubwa cha mshahara wa paundi 170,000 ambacho alikuwa akilipwa wakati akiwa katika klabu ya City alipojiunga nayo katika kipindi cha majira ya kiangazi mwaka 2009. Hata hivyo City nao watakuwa wamepata hasara kubwa kwa mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Togo ambaye walimnunua kutoka klabu ya Arsenal kwa ada ya paundi milioni 25. Kwasasa meneaj wa City anajipanga kutumia mwanya wa kumuuza Adebayor kujaribu kumnyakuwa kiungo Javi Martinez ambaye anataka kwenda klabu ya Bayern Munich ya Ujerumani akitokea klabu ya Athletic Bilbao ya Hispania.

No comments:

Post a Comment